Posts

Showing posts from February, 2022

Manchester United imesitisha mkataba wake wa udhamani na kampuni ya ndege ya Urusi

Image
 Klabu ya Manchester United imesitisha mkataba wake wa udhamani na kampuni ya ndege ya Urusi Aeroflot wenye thamani ya Pauni milioni 40, kufuatia Urusi kuvamia nchini Ukraine. Manchester United wamekuwa na mkataba wa wakusafirishwa na shirika hilo tangu mwaka 2013

KISINDA TUTAIPIGA SIMBA NYINGI

Image
 KISINDA  TUTAIPIGA SIMBA NYINGI Yule winga wa zamani wa Yanga SC 🇹🇿 kwenye kasi ya kishada, Tuisila Kisinda 🇨🇩 ambaye sasa anaitumikia klabu ya RS Berkane 🇲🇦, ameipiga mkwara Simba SC 🇹🇿 akidai hasira ya kipigo walichopewa na Asec Mimosas 🇨🇮 zitaishia kwao wakati timu hizo zitakapokutana katika mechi itakayopigwa Jumapili hii. Kisinda amesema: “Simba SC 🇹🇿 nawajua ni wazuri na matokeo waliyoyapata ugenini yamewapa nguvu, lakini nasi tumejipanga na tunataka  ushindi dhidi yao bila kuangalia idadi ya mabao, tutawapiga.” alisema Kisinda ambaye kasi yake iliwasumbua sana mabeki wa Simba SC 🇹🇿 katika Kariakoo Derby.

𝐇𝐀𝐊𝐔𝐍𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐙𝐔𝐈𝐀 𝐑𝐎𝐁𝐎 𝐅𝐀𝐈𝐍𝐀𝐋𝐈 𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈𝐒𝐇𝐎 - 𝐓𝐑𝐘 𝐀𝐆𝐀𝐈𝐍

Image
 𝐇𝐀𝐊𝐔𝐍𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐙𝐔𝐈𝐀 𝐑𝐎𝐁𝐎 𝐅𝐀𝐈𝐍𝐀𝐋𝐈 𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈𝐒𝐇𝐎 - 𝐓𝐑𝐘 𝐀𝐆𝐀𝐈𝐍 ➪Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah Muhene 'Try Again' amesema kwa mikakati waliyojiwekea, basi ngumu kutokea timu ya kuwazuia kufuzu hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. ➪Simba wameipata jeuri hiyo baada ya kukaa kileleni katika Kundi D wakikusanya pointi nne mbele ya ASEC Mimosas, RS Berkane na US Gendarmerie. ➪Akizungumza baada ya Simba kupata sare ya 1-1 ugenini dhidi ya US Gendarmarie, Try Again alisema usiri mkubwa uliokuwepo kambini baada ya baadhi ya wachezaji kuugua ghafla, ulichangia kwa kiasi kikubwa wao kupata matokeo mazuri ugenini ➪Try Again alisema kabla ya mchezo huo, wachezaji wao akiwemo Jonas Mkude, aliugua ghafla, lakini hakuna mtu kutoka nje ya kambi hiyo ambaye alifahamu na kuwafanya wapinzani wakutane na sapraizi uwanjani ➪"Haikuwa kazi rahisi kupata matokeo haya hapa ugenini, vijana wetu walipambana sana kutoka...

UEFA imehamishia fainali ya UEFA Champions League

Image
 Official:  UEFA imehamishia fainali ya UEFA Champions League kutoka St Petersburg (Urusi) hadi Paris (Ufaransa) kufuatia mzozo wa Urusi dhidi ya Ukraine.   Fainali itafanyika kwenye Uwanja wa Stade de France Jijini Paris, Mei 28.

Gianni Infantino ametangaza kuvifungia kwa muda usiojulikana vyama vya Soka Nchini Kenya na Zimbabwe

Image
 Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino ametangaza kuvifungia kwa muda usiojulikana vyama vya Soka Nchini Kenya na Zimbabwe kufanya shughuli za Mpira wa Miguu  Kutokana na kuingiliwa na Serikali katika uendeshaji wa Masuala ya soka.   #FIFA #kenya #Zimbabwe🇿🇼

Mashabiki Ruksa Kushuhudia Rs Berkane Vs Simba Sc

Image
 -Shirikisho la soka Afrika CAF limeruhusu watazamaji kwenye mchezo wa RS Berkane dhidi ya Simba SC utakaopigwa Feb 27 Ikumbukwe mashabiki nchini Morocco walizuiliwa kuingia uwanjani tangu mlipuko wa Covid 19 kutokana na idadi ya visa vya Covid kuwa vingi nchini humo.

IBENGE: TUTAWATULIZA MORRISON NA SAKHO

Image
 IBENGE: TUTAWATULIZA MORRISON NA SAKHO Kocha wa Berkane, Mkongomani Florent Ibenge amefunguka kuwa kikosi chake kina mtihani mkubwa kuanza kutafuta dawa ya kuwatafutia tiba viungo washambuliaji wawili wa wekundu wa Msimbazi, Pape Sakho na Bernard Morrison ndio mastaa wawili wanaotakiwa kutafutiwa tiba ya kuwatuliza wakati huu beki yao imekuwa na makosa makubwa. . “Simba ni timu kubwa, tunakabiliwa na mchezo mgumu dhidi yao, ukiangalia katika mechi zao mbili kuna watu ambao kama tunataka kushinda lazima tuwatafutie mbinu za kuwatuliza,” amesema Ibenge. . “Sakho (Pape) ni mchezaji mwepesi anayehitajika kuangaliwa sana kwa jinsi taarifa za mechi zao nilivyozipata lakini kuna yule Morrison (Bernard) ni mchezaji mzuri mwenye ubora akiwa uwanjani achilia mbali nidhamu yake, namjua vyema ni lazima tuwe na akili ya kuwazuia. . “Shida yetu ni makosa ambayo mabeki wangu wameyafanya kwenye mechi hizi mbili ni lazima tujue kucheza kwa utulivu kabla ya kukutana na Simba makosa haya ndio yametu...

No War In Ukraine Ruslan Malinovskyi

Image
 “No war in Ukraine” - Huo ni ujumbe wa kiungo wa kimataifa wa Ukraine anayechezea Atalanta,Ruslan Malinovskyi baada ya kufunga goli kwenye mchezo wa Europa League dhidi ya Olympiacos usiku huu.

Timu zilizocheza faulo nyingi Ligi Kuu Ya NBC

Image
 Timu zilizocheza faulo nyingi zaidi katika mechi (15) za duru la kwanza ligi kuu. 01. ⚠️ 256 = Geita gold. 02. ⚠️ 246 = Mbeya city. 03. ⚠️ 232 = Dodoma jiji. 04. ⚠️ 217 = Kagera sugar. 05. ⚠️ 213 = Tanzania Prisons. 06. ⚠️ 212 = Namungo fc. 07. ⚠️ 204 = Mbeya kwanza. 08. ⚠️ 197 = Coastal Union. 09. ⚠️ 193 = Ruvu shooting. 10. ⚠️ 187 = KMC. 11. ⚠️ 186 = Polisi Tanzania. 12. ⚠️ 182 = Azam fc. 13. ⚠️ 182 = Mtibwa sugar. 14. ⚠️ 169 = Biashara United. 15. ⚠️ 156 = Simba sc. 16. ⚠️ 118 = Young Africans sc Credit to @Azam Tv

BAADA YA URUSI KUISHAMBULUA UKRAINE KIJESHI…..

Image
 BAADA YA URUSI KUISHAMBULUA UKRAINE KIJESHI….. Poland, Uswisi na Jamhuri ya Czech zimetoa kauli ya pamoja ya KUKATAA kucheza mechi zao za mchujo za Kombe la Dunia la FIFA dhidi ya Urusi huko Moscow. Hali ambayo imezidi kuiweka rehani Urusi katika michuano ya kimataifa na uanachama wake FIFA. Mpaka sasa bado FIFA hawajatoa tamko lolote kuhusu ushiriki wa Urusi kisoka duniani baada ya taifa hilo kuivamia kijeshi Ukraine kwa makombora na roketi.  Tayari nchi mbalimbali Ulaya magharibi na Marekani wameiwekea vikwazo Urusi na kukataa ushirikiano nayo katika michezo.

Ni Kocha Wa Simba Sc Pablo Vs Kocha Wa ZamalekPatrice Carteron

Image
 ✍️ Pichani ni Kocha wa Simba Pablo Franco 🇪🇦 akiongea na Kocha wa Zamalek Patrice Carteron 🇫🇷 Jana jioni kabla ya mazoezi ya Simba. ♦️Kuna eneo Simba wako bora sana... Wana mahusiano mazuri na vilabu vikubwa na wana watu sahihi sana wa Logistics ♦️Ni kwakuwa tumechagua kuwadharau Simba Sc...ila Simba kwa sasa ina jina kubwa sana nje ya mipaka ya Nchi. Natamani timu zingine kama Yanga, Azam na kina Namungo wajifunze kwa Simba Sc. ♦️Ni nadra sana kuona yale yaliyowakuta Namungo pale Angola,Azam kule Swaziland ama Yanga walipokuwa Nigeria yakiwakuta Simba Sc.  ♦️Sikiliza...wale kina Victorien Adebayor na Wilfred Gbeuli wa USGN walikiri wao kwa nyakati tofauti kuwa Simba ni timu kubwa. ♦️Mara kadhaa waandishi wakubwa Afrika kama Lorenz Kohler na Nuhu Adams wamekuwa wakitoa takwimu za ukubwa wa Simba ambazo sisi wabongo wenyewe sometimes tunazikataa. ♦️Hata taarifa zilizosambaa kuwa Simba walilala Airport ni kwa vile tu wabongo tuna utamaduni wa kuzungumza tusiyoyajua ♦️Simba ...

Chris Mugalu Kumpisha Adebayor

Image
 -Uongozi wa Simba umethibitisha kuachana na staa mmoja mkubwa wa kigeni katika timu hiyo ili kiungo mshambuliaji wa US Gendarmerie ya nchini Niger, Mnigeria, Victorien Adebayor achukue nafasi yake. -Tetesi zinasema kuwa, mshambuliaji Mkongomani, Chris Mugalu, ndiye anayetajwa kuachwa kutokana na kuwa na matatizo mengi ikiwemo majeraha ya mara kwa mara.

Golikipa Wa Zamalek Akutana Na Wachezaji Wa Simba Sc

Image
 -Yule golikipa 'Jini' waliekuwa wanamuona kwenye Tv akipangua penati ya Sadio Mane kwenye michuano ya AFCON iliyofanyika nchini Cameroon hatimaye wamekutana nae live Yes, Mohamed Aboul Gabal 'GABASK' jana alikutana na magolikipa wa Klabu ya Simba nchini Morocco. Gabaski ambaye ni golikipa wa Zamalek ni miongoni mwa magolikipa bora sana kwasasa Barani Afrika.

Baada ya (TFF) kutoa orodha ya mawakala wa wachezaji Shafii Dauda Aibuka

Image
 - Baada ya (TFF) kutoa orodha ya mawakala wa wachezaji  wanaotambulika na ambao wanaruhusiwa kufanya kazi nchini...... ..... Huku majina ya Shaffih Dauda na Jemedari Said yakikosekana, wachambuzi hao wameeleza yafuatayo ; "Mimi sio wakala, na sijawahi kuwa na leseni ya uwakala. Namiliki kampuni ya uwakala SHADAKA ambayo ilikuwa na wakala Ibrahim Mohamed ambaye kwa sasa haja-RENEW leseni yake" 🔍 Shaffih Dauda. "Kazi yangu ni kuwakutanisha vijana na mawakala wakubwa mbalimbali" 🔍 Shaffih Dauda. . . "Alichoeleza Shaffih ndivyo ilivyo,, unauliza mimi ni wakala au meneja ?  Ofcoz mimi ni Meneja sio wakala" "Kama meneja wa Aishi Manula tulifanya kazi na wakala FAUSTINO IKANDILA, kuna timu ilimuhitaji Manula lakini wakala huyo akahitaji pesa nyingi zaidi kutoka kwa klabu hiyo klabu ikasitisha dili" 🔍 Jemedari Said. "Sasa hivi tulishajitoa kwa wakala huyo kwa sababu tuliona mkataba baina yetu hauna faida. Miimi ni meneja wa Aishi Manula, John Bo...

LEVY Vs CONTE

Image
 LEVY Vs CONTE  Daniel Levy alimpata Mauricio Pochettino ambaye aliikuta Spurs ambayo ipo dhofu bin hali, Muargentina huyo akaibadilisha Spurs bila kutumia pesa nyingi mpaka kuwa timu ya Top 4 na ilikaribia kutwaa taji la EPL ( Mwaka ambao Leicester alikuwa bingwa ) akimaliza nafasi ya 3 - Ilifika wakati Net Spend ya Spurs ilikuwa Pauni Milioni 38 ( Yani ulichotumia na ulichoingiza tofauti yake kwenye usajili ) ni hela ndogo sana tofauti na ilivyokuwa dhidi ya City Liverpool United Chelsea na Arsenal lakini bado Spurs walikuwa Top kwao ipo chini ya Pochettino .  Levy mkono wake wa birika alishindwa kumuunga mkono Pochettino , mwaka 2018 dirisha la usajili la majira ya kiangazi Spurs hawakusajili hata mchezaji mmoja na bado walifika fainali ya UCL 2018/2019.  Akaja Jose Mourinho , kocha ambaye anapenda wachezaji ambao tayari wameiva ili akupe makombe ( amefanya hivyo vilabu vingi ) lakini hadithi ilikuwa ile ile , Spurs waliamua kusajili wachezaji wa bei chee sana na ...

Mpya kutoka UEFA..

Image
 Mpya kutoka UEFA..  UEFA itatangaza kesho kwamba kuhusu kuhamishwa fainali ya UEFA Champions League kutoka Saint Petersburg (Urusi).  Source : Sky Sports

Jamie Carragher kuhusu Rashford:

Image
 Jamie Carragher kuhusu Rashford: “Marcus Rashford amekuwa kwenye timu hii (Man United) tangu akiwa mtoto na mara zote alikuwa akipambana kwenda ngazi ya juu, ambapo wachezaji wa juu wanafika, lakini bado hajafika huko.”  “Sasa tumefikia mahali ambapo sidhani kama anafaa kuwa kwenye kikosi cha kwanza cha Manchester United. Uchezaji wake msimu huu haumhakikishii kuwa kwenye timu.” “Mara nyingi anakuwa kwenye kikosi cha kwanza, hata wachezaji wengine wanapokuwa fiti yeye anapewa nafasi, uhusika wake upande wa kulia haumfai hata kidogo, hivyo anatakiwa awe kushoto au ndani. katikati.”  “Lakini bado tunasubiri Rashford achukue hatua hiyo na kuwa mchezaji mkubwa wa United au mchezaji ambaye anaweza kuwasaidia kushinda mataji makubwa, na yeye bado hajafikia hapo.”  “Katika umri huu, United inahitaji mtu bora kuliko Marcus Rashford wa sasa.”

Athari za mzozo wa Urusi na Ukraine katika Soka

Image
 Athari za mzozo wa Urusi na Ukraine katika Soka .Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich amezuiwa kabisa kuishi Uingereza kwa vile anatajwa kuwa mmoja wa wawezeshaji wakuu wa utawala wa Rais wa Urusi Vladimir Putin. .Ligi za Soka nchini Ukraine zimesimama kwa muda wa mwezi mmoja kutokana na mzozo wa kisiasa ulipo kwa sasa kati ya Nchi hiyo na Urusi. .UEFA wanajadili uwezekano wa kuhamisha fainali ya UEFA Champions League msimu huu kutoka St Petersburg (Urusi) kutokana na mzozo huo.

Mchezaji Wa Timu Ya England Abadili Uraia Wake Na Kuwa Mtanzania

Image
 DONE & CONFIRMED 📌 Beki wa kushoto ambaye pia hucheza beki wa kati katika Klabu ya Portmouth inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza 'Championship' Nchini Uingereza,Haji Mnoga amekubali kubadili uraia na kuwa Mtanzania Rasmi baada ya Hatua zote kufuatwa na kukamilika. Mnoga mwenye umri wa miaka 19 amewahi kuitumikia timu ya Vijana ya England Chini ya Miaka 17 na 19 na sasa anaruhusiwa kuitumikia timu ya Taifa ya Tanzania endapo ataitwa. HONGERA & KARIBU SANA @mnogsss

Florent Ibenge Sina Record Nzuri Kw Simba Sc

Image
 🗣 " Ni kweli rekodi yangu dhidi ya Simba si nzuri lakini sio sababu ya sisi kufeli dhidi yao. Tuna nafasi nzuri ya kupambana dhidi yao, tumetoka kupoteza katika mchezo uliopita tukiwa ugenini nchini Ivory Coast hivyo tunatakiwa kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani. Kwa jinsi ilivyo ni lazima tupate matokeo nyumbani." Kocha wa RS Berkane, Florent Ibenge akisisitiza ni lazima wapate matokeo katika mchezo ujao dhidi ya Simba.

RATIBA YA SOKA LEO JUMATANO.

Image
 RATIBA YA SOKA LEO JUMATANO. TANZANIA - NBC Premier League 16:00 Mtibwa Sugar vs Yanga SC  ENGLAND: Premier League 22:30 Burnley vs Tottenham  22:30 Watford vs Crystal Palace  22:45 Liverpool vs Leeds  EUROPE: Champions League - Play Offs 23:00 Atl. Madrid vs Manchester Utd  23:00 Benfica vs Ajax  AFRICA: CAF Confederation Cup 16:00 Otoho d'Oyo (Con) vs Cotonsport (Cmr)  AFRICA: African Championship Women - Qualification 17:30 Gabon W vs Togo W  18:00 Equatorial Guinea W vs Tunisia W  18:00 Gambia W vs Cameroon W  18:00 Ivory Coast W vs Nigeria W  19:00 Burkina Faso W vs Guinea Bissau W  20:00 Algeria W vs South Africa W  20:00 Botswana W vs Zimbabwe W  20:00 Mali W vs Senegal W  BELGIUM: Jupiler Pro League 20:45 Gent vs Seraing  EGYPT: Premier League 16:00 Eastern Company vs Al Masry  18:30 El Ismaily vs El Gouna  ENGLAND: Championship 22:45 Derby vs Millwall  22:45 Fulham vs Peterborou...

Azam fc wamepigwa na kitu kizito 🙆

Image
 Azam fc wamepigwa na kitu kizito 🙆 Full 🕡 Biashara Utd  2 - 0  Azam fc 49'  🕡 Collins Opare ⚽ 🔥 90' + 2 🕡 James Shagara ⚽, Note ; Huyu Collins Opare aliichukua cleansheet ya Diarra juzi juzi kwenye (FA). Usajili bora wa dirisha dogo 💪 Msimamo wa ligi kuu Tanzania bara. 1. 👕 14 ⚽ 19 🅿️ 36 = Young Africans. 2. 👕 15 ⚽ 10 🅿️ 31 = Simba SC. 3. 👕 15 ⚽ 07 🅿️ 24 = Azam fc. 4. 👕 15 ⚽ 05 🅿️ 23 = Namungo fc. 5. 👕 15 ⚽ 04 🅿️ 23 = Mbeya city.

Kutoa Mimba Sasa Ruksa

Image
 Colombia imekuwa Nchi ya 4 kutokea Amerika Kusini kuhalalisha utoaji mimba kwa Wanawake, hii ni baada ya Mahakama ya Kikatiba ya taifa hilo kupiga kura ya kuhalalisha utoaji wa mimba hadi wiki ya 24 ya ujauzito. Sio Watu wote walioikubali sheria hii na sio wote walioipinga, wengi wa waliokubaliana nayo wanasema itasaidia Wanawake laki nne kila mwaka kuachana na mimba ambazo wamezipata kinyemela ikiwemo kwenye vitendo vya kubakwa. Kabla ya uamuzi huu, Colombia ilikua inaruhusu utoaji mimba wakati tu maisha ya Mwanamke yapo hatarini au kama ujauzito uliotokana na ubakaji lakini sasa kwenye sheria hii mpya Wanawake wa Colombia wataweza kutoa mimba hadi wiki ya 24 ya ujauzito wao bila kutoa sababu zozote na itakua ni uamuzi wao. Nchi nyingine za Amerika ya Kusini ambazo jambo hili limehalalishwa ni Argentina, Uruguay na Cuba ambazo huruhusu utoaji wa mimba bila vikwazo hadi hatua fulani za ujauzito.

Seleman Matola Wamuachie Simba Sc Awe Kocha Mkuu

Image
 “Hii Simba mnayoiona, wakiamua kumuachia Seleman Matola awe Kocha Mkuu, timu itaenda vizuri tu bila wasiwasi wowote, ni suala la viongozi tu kuamua.” MECKY MEXIME.  WANA-SIMBA MNASEMAJE? AACHIWE MATOLA AU?

Mchezaji ASiyeona Galatasaray

Image
 Mwaka 2020 beki wa klabu ya Galatasaray 🇹🇷 Omar Elabdellaouri alipoteza uwezo wa kuona baada ya kulipukiwa na fataki. - Ilimchukua takribani mara (11) kufanyiwa surgery kurejesha uwezo wake wa kuona 👀. - Leo kwa mara ya kwanza baada ya siku (423) amerejea na kucheza soka katika klabu yake ya Galatasaray 🇹🇷 🙏 NB ; Omar ni huyo aliyevaa miwani.

Somalia Vs Eswatini Kukipiga Kwa Mkapa

Image
 Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Somalia (SFF) limetangaza kuwa watacheza mchezo wao wa awali wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (#AFCON) 2023 dhidi ya Eswatini jijini Dar es Salaam, Tanzania. Hii ni kwa sababu hawana Uwanja wowote ulioidhinishwa kucheza mechi ya kimataifa.

Yalipo Mafanikio Ya Simba Sc Yupo Shomari Kapombe

Image
 Unapozungumzia mafanikio ya Simba SC kwa miaka ya hivi Karibuni lazima utaje jina la Shomari Kapombe, Enock  Bwigane alimbatiza jina la "Show me the way". Nyota huyu aliyekuzwa katika nyumba ya vipaji ya Moro kids pale Morogoro, ni moja ya mabeki Bora kabisa wa upande wa kulia kuwahi kutokea Afrika Mashariki kwa kizazi hiki cha sasa. Shomari Kapombe sifa yake kubwa ni kuwa na mapafu ya mbwa,  akipandisha mashambulizi kwa kasi kubwa na kurudi kuzuia kwa wakati,  kila Wapinzani wanapolishambulia lango la Simba SC.Hali hii imemfanya awe kipenzi cha mashabiki wa Soka hapa Nchini. Kama haitoshi Kapombe hajui kuzuia tu bali pia ana uwezo mkubwa wa kupiga pasi za mwisho kwa washambuliaji ili wafunge na yeye akipata nafasi huweka Mpira kimiani bila ajizi.  Hii inamfanya awe Beki wa kulia wa  kisasa kabisa kwa sasa huku akilinganishwa sifa zake na Kyle Walker nyota  wa Man City aliyebora  wakati wa kuzuia na pia ni hatari wakati wa kutengeneza shambulizi,...

REKODI ZA MBWANA SAMATTA MSIMU HUU AKIWA NA ROYAL ANTWERP: .

Image
 🇹🇿 | REKODI ZA MBWANA SAMATTA MSIMU HUU AKIWA NA ROYAL ANTWERP: . ⌾ Ligi Kuu ya Ubelgiji 🏟 22 Mechi. ⚽️ 04 Mabao. 🎯 03 Assists. ⌾ UEFA Europa League 🏟 6 Mechi. ⚽️ 3 Mabao. 🎯 0 Assists.

MWAKALEBELA:YANGA TOP 10 AFRIKA. TUNAINGIA.

Image
 MWAKALEBELA:YANGA TOP 10 AFRIKA. TUNAINGIA. “Sasa tunataka tuwe katika nafasi 10 bora Afrika, huko chini tumeshavuka. Watanzania bila kujali ushabiki tuendelee kuiombea Yanga ili izidi kufanya vizuri kwa msimu ujao tutaibebe nchi kimataifa na malengo yetu ni kuhakikisha tumeingia katika vilabu 10 Bora Afrika.” Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, FREDRICK MWAKALEBELA.

Utata Wa Umri Wazidi Kuibua Mengi

Image
 Ana miaka 15 na miezi 9 akiwa na medali ya ushindi baada ya kushinda tuzo kwa soka la vijana chini ya umri wa miaka 16 ndani ya taifa la DRC 🇨🇩. 😢

MASHABIKI 50 WAKWANZA KUCHANJA KUSHUHUDIA MECHI KATI YA BIASHARA MARA NA AZAM FC BURE.

Image
  MASHABIKI 50 WAKWANZA KUCHANJA KUSHUHUDIA MECHI KATI YA BIASHARA MARA NA AZAM FC BURE. Na WAF - Mwanza Kuelekea mchezo unao tarajiwa kuchezwa siku ya jumanne ya terehe 22 februari 2022 kati ya Biashara mara na Azam fc mashabiki wa mpira na wananchi wa mkoa wa Mwanza kwa ujumla washauriwa kupata chanjo dhidi ya Uviko -19 na wananchi 50 wakwanza watakao chanja kupata fursa ya kushuhudia mechi hiyo bila kiingilio, Yamesemwa hayo leo katika uwanja wa CCM kirumba na katibu msaidizi - chama cha soka mkoa wa Mwanza Bw. Khalid Bitebo akiongea na vyombo vya habari juu ya mchezo huo utakao chezwa kesho uwanjani hapo, Bw Khalid Bitebo amesema wananchi na mashabiki wa mpira wa miguu wajitokeze kwa wingi kupata chanjo dhidi ya Uviko - 19 ili kujikinga na kuwakinga wengine dhidi ya ugonjwa huo, "Tunapenda kuwapa taarifa kwamba Kesho kutakuwa na zoezi la kuchanja chanjo ya Uviko - 19 katika uwanja wa CCM kirumba na wananchi 50 wakwanza watakao chanja watapata fursa ya kuingia uwanjani bure bil...

Lusajo Ni Mwendo Wa Kimya Kimya Wataelewa Tu

Image
 😮 E bana ee ! Lusajo amefunga magoli mengi ligi kuu (⚽10) msimu huu kuliko magoli yote waliyofunga Tanzania Prisons ligi kuu msimu huu mpaka sasa 🔥 Full 🕡 Namungo fc  2 - 0  Mbeya city. 40'  🕡 Lukas Kikoti ⚽ 47'  🕡 Reliants Lusajo ⚽ Note ; Mbeya city wamepoteza mchezo wa pili ligi kuu msimu huu. Ni Yanga SC pekee ambao hawajapoteza mchezo. 1. ❌ 00 = Young Africans. 2. ❌ 02 = Mbeya city. 3. ❌ 03 = Simba SC Namungo wamemtoa Mbeya city kwenye nafasi ya (4) ligi kuu Tanzania bara. 1. 🎱 14 ⚽ 19 🅿️ 36 = Young Africans. 2. 🎱 15 ⚽ 10 🅿️ 31 = Simba SC. 3. 🎱 14 ⚽ 08 🅿️ 24 = Azam fc. 4. 🎱 15 ⚽ 05 🅿️ 23 = Namungo 5. 🎱 15 ⚽ 04 🅿️ 23 = Mbeya city. 6. 🎱 15 ⚽ 00 🅿️ 20 = Geita gold
Image
 KUNA MAHALA YANGA WANAKWAMA ➡️ Klabu ya Yanga ya jijini Dar-es-salaam imetangaza kuwa inaongoza kwa mauzo ya jezi mara tano kuliko klabu yeyote na wakati huohuo imeshusha bei ya jezi hizo kutoka bei ya jumla jumla ya zamani Tsh 30,000/= hadi Tsh 22,000 na kwa bei ya rejareja kutoka 35,000/= hadi 30,000/= ➡️ Jambo la kujiuliza inakuwaje ushushe bei ya bidhaa inayonunuliwa zaidi sokoni tena kwenye kipindi ambacho inauzika kuliko jezi nyingine yeyote? ➡️ Yaani ni sawa na kusema una duka la nafaka kama mchele,ngano, maharage halafu kati ya bidhaa hizo mchele ndio unanunuliwa kwa kasi mara tano ya ya bidhaa nyingine hapo dukani na mchele huo huo uushushe bei  ➡️Kama hii sio kazi ya Manara basi idara ya masoko hapo jangwani haipo sawa huu mmetuletea mchezo wa kitoto NB: WAKATI WENGINE WAKIHANGAIKA KUMNUNUA ADEBAYOR YANGA HUKU WANAHANGAIKA KUMNUNUA MARIOO NDIO MAANA WIMBO WA POMBE UMEGEUZWA KUWA WIMBO WA YANGA

Harmonize Mniite Bakhresa

Image
 Msanii  Harmonize amewataka mashabiki wake kumuita jina la Bakhresa kuanzia leo. Kupitia ukurasa wake wa instagram Harmonize ameandika Call Me Bakhresa from today”

Haji Manara Jezi Ya Kuuzwa Elfu 22 Tu

Image
 "Tumetoa punguzo la bei kwenye jezi za Yanga ili mashabiki wengi wapate jezi original kwa bei ndogo na kuongeza hamasa. Reja reja zitauzwa Tsh 30.000/= na jumla Tsh 22,000/ =" "Kwa mujibu wa takwimu, Yanga mpaka sasa imeuza jezi mara tano ya vilabu vingine Tanzania msimu huu" 🔍 Haji Manara msemaji wa Yanga.

Yanga Yazindua Wimbo Mpya .

Image
 Klabu ya Yanga SC imezindua wimbo mpya unaofahamika kama 'YANGA TAMU'.Wimbo huo umeimbwa na Mwanamuziki MARIOO ambaye anatamba na wimbo wa BIA TAMU. ✍️Ikumbukwe Marioo alikuwa Simba sc na mara kazaa alikuwa akishiriki katika matamasha ya Simba sc Marioo mwenye anasema kuwa sababu ya kuhama Simba sc ✍️Ni Kuwa hapendi stress hataki presha wala magonjwa ya moyo na ndomaana kahamia Yanga sc ✍️ @marioo_tz alitambulishwa na mwamasishajii wa klabu ya yanga Haji Manara ambaye pia alitambulisha wimbo kwa ajili ya mashabiki ambao umeimbwa na marioo wimbo unaitwa "Yanga Tamu" akibadilisha wimbo wake wa  Bea Tamu "Wimbo huu ni kwa ajili ya mashabiki wa" yanga sc @hajismanara  WANANCHI KAMA WANANCHI..

KAULI 4 ZA BIN ZUBEIRY KWA YANGA NA SIMBA

Image
 KAULI 4 ZA BIN ZUBEIRY -Yanga sio timu yenye ubora wa kucheza mashindano ya CAF” - Bin Zubeiry -Ligi ya NBC sio miongoni mwa ligi bora barani Afrika, kama nchi tulipeleka timu nne lakini mpaka sasa imebaki Simba tu” - Bin Zubeiry -Nchi ambazo zina ligi bora, zina timu zaidi ya moja kwenye hatua y’a makundi ya michuano ya CAF, kwa hapa Tanzania kuna timu zingine alafu kuna Simba” - Bin Zubeiry -Simba wameseti standard yao ambayo inaitofautisha kwa mambo mengi na vilabu vingine, linapokuja suala la Mashindano ya kimataifa, Watanzania tuungane kwa pamoja kuisapoti Simba, ndiyo inayotuwakilisha vizuri” - Bin Zubeiry

🚨AZAM SPORTS FEDERATION CUP 🏆 HATUA YA ROBO FAINALI.

Image
 DRAW YA AZAM SPORTS FEDERATION CUP  Robo Fainali  👉89 Yanga SC vs Geita Gold FC  👉90 Simba SC vs Pamba SC  👉91 Azam FC vs Polisi Tanzania  👉92 Coastal Unions vs Kagera Sugar  Nusu fainali  👉93 Yanga/Geita vs Simba/Pamba        Uwanja :- CCM Kirumba Mwanza  👉94 Azam/Polisi vs Coastal/Kagera       Uwanja :-Shikh Amri Abeid Arusha Fainali  👉95 Winners Sem Final #AzamSportsFederationCup

Masau Bwire Awapa Neno Simba Sc

Image
 Ameandika Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire "Nawashukuru, nawapongeza sana wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wapenzi, wadau, mashabiki wa Ruvu Shooting FC na Simba SC, kadharika Watanzania wote Wazalendo, kwa kufanya vyema katika michezo yao iliyochezwa Februari 20, 2022, timu zote zikiwa ugenini. Ruvu Shooting ikicheza na Tanzania Prisons, ligi ya NBC, uwanja wa Sokoine, Mbeya, ikashinda goli 0-1 dhidi ya Tanzania Prisons, imetoka nafasi ya 15 ya msimamo hadi ya 12. Simba SC, wakicheza hatua ya makundi, kombe la Shirikisho Afrika na timu ya USGN huko Niger, iliwalazimisha wenyeji hao sare ya goli 1-1, matokeo ambayo yameifanya iongoze kundi kwa pointi 4. Watanzania wazalendo, tuendelee kuiombea Simba SC, iendelee kufanya vizuri katika michezo ijayo ya mashindano hayo ya Shirikisho Afrika, ili izidi kuitangaza nchi kiuchumi, lakini pia zaidi sana katika ubora wa soka. Wengi walidhani Ruvu Shooting ni timu dhaifu ilipofungwa na Simba SC magoli 7-0, bila kujua ilikuwa ikip...

BARBRA: KILA KITU KIPO TAYARI MOROCCO .

Image
 BARBRA: KILA KITU KIKO TAYARI MOROCCO  . CEO wa Simba Barbara Gonzalez ambaye tayari yupo nchini Morocco 🇲🇦 amesema mambo yako sawa ili kuhakikisha timu inaenda kufanya vizuri ugenini. . Amefafanua kuwa wamefanya uchunguzi na tayari wamekamilisha suala la usafiri, sehemu ya kufikia na chakula. 👏

Wanawake Mpo Hii Ni Hatari Sana

Image
 HII NI HATARI Kuna ugonjwa unaitwa gangrene, husababishwa na kukosekana au kutofika kwa damu kwenye sehemu fulani ya mwili. Damu hukosekana kwa sababu nyingi, ikiwemo kubanwa kwa mishipa ya usambazaji kutokana na uvaaji wa viatu kama hivi. Mishipa inayosambaza damu mwilini ikibanwa sana, inashindwa kufikisha damu katika maeneo yaliyobanwa. Damu inapofika sehemu mbalimbali za mwili, husambaza hewa ya oksijeni na virutubisho muhimu kwa afya ya binadamu. Pia huupatia mfumo wa kinga mwilini viatilifu (antibodies) kusaidia kupambana na maambukizi ya maradhi mbalimbali. Damu inaposhindwa kusambaa vizuri mwilini, seli za eneo husika haziwezi kuendelea kuwa hai na tishu za sehemu hiyo huoza. Kuoza kwa tishu za eneo lililoathirika husababisha kubadilika rangi na kuwa ya zambarau, kahawia, bluu au nyeusi. Gangrene ni ugomjwa hatari sana !

MATOKEO YA SOKA JANA JUMAPILI.

Image
 MATOKEO YA SOKA JANA JUMAPILI. TANZANIA: Ligi Kuu Bara FT Tanzania Prisons 0-1 Ruvu Shooting  FT KMC FC 2-0 Dodoma Jiji  ENGLAND: Premier League FT Leeds 2-4  Manchester Utd  FT Wolves 2-1 Leicester  FRANCE: Ligue 1 FT Nice 1-0 Angers  FT Lorient 0-1 Montpellier  FT Reims 1-1 Brest  FT Rennes 4-1 Troyes  FT St Etienne 2-2 Strasbourg  FT Bordeaux 1-1 Monaco  FT Marseille 0-2 Clermont  GERMANY: Bundesliga FT Bayern Munich 4-1 Greuther Furth  FT Dortmund 6-0 B. Monchengladbach  FT Hertha Berlin 1-6 RB Leipzig  ITALY: Serie A FT Fiorentina 1-0 Atalanta  FT Venezia 1-1 Genoa  FT Inter 0-2 Sassuolo  FT Udinese 1-1 Lazio  NETHERLANDS: Eredivisie FT Zwolle 1-1 Groningen  FT Feyenoord 3-1 Cambuur  FT Twente 2-2 G.A. Eagles  FT PSV 3-1 Heerenveen  FT Utrecht 1-1 Vitesse  TURKEY: Super Lig FT Gaziantep 0-3 Adana Demirspor  FT Alanyaspor 0-4 Trabzonspor  FT Karagum...

RATIBA YA SOKA LEO JUMATATU.

Image
 RATIBA YA SOKA LEO JUMATATU. TANZANIA: Ligi Kuu Bara 16:00 Namungo vs Mbeya City ITALY: Serie A 21:00 Cagliari vs Napoli  23:00 Bologna vs Spezia  SPAIN: LaLiga 23:00 Celta Vigo vs Levante  AFRICA: African Championship Women - Qualification 22:00 Algeria W - South Africa W  20:00 Botswana W vs Zimbabwe W  20:00 Burkina Faso W vs Guinea Bissau W  20:00 Djibouti W vs Burundi W  20:00 Equatorial Guinea W vs Tunisia W  20:00 Gabon W - Togo W  20:00 Gambia W - Cameroon W  20:00 Ivory Coast W - Nigeria W  20:00 Kenya W - Uganda W  22:00 Mali W - Senegal W  22:00 Namibia W - Zambia W  EGYPT: Premier League 21:30 Arab Contractors vs Smouha  21:00 El Gaish vs Pharco  RWANDA: Premier League 16:00 APR vs Etincelles  16:00 Bugesera FC vs Rayon Sport  16:00 Musanze vs Etoile de L'Est   TURKEY: Super Lig 20:00 Goztepe vs Galatasaray ZIMBABWE: Premier Soccer League 16:00 CAPS Utd vs Ngezi Platinum...

Salim Abdallah Try again Victor Adebayor Anakuja Simba Sc.

Image
 Mwenyekiti wa bodi ya Simba sc ! "Huyu (Victorien Adebayor) ni mchezaji mzuri sana, niliongea na Rais wa klabu ya USGN 🇳🇪 akaniambia yuko hapa kwa mkopo akitokea Denmark 🇩🇰,, Huyu si mchezaji wa kurudi Denmark anatakiwa kucheza Simba SC... Nitaongea na Rais tuvunje benki"  "Simba sports club ni timu kubwa barani Africa, kwa nini isiwezekane !!"  🔍 Salim Abdallah Try again.

Bernard Morison Aipa

Image
 FT' US Gendarmerie 1-1 Simba SC      12' Wilfred                  84' Morrison  FT' Asec Mimosas 3-1 RS Berkane       58' Aziz Ki                  84' El Bahri      65' Coulibly       70' Konate   Msimamo  Kundi D                                  P.     GD.   Pts.  1-Simba SC             2       2       4 2-Asec Mimosas    2       0       3  3-RS Berkane          2       0       3 4-Us Gendarmerie  2      -2       1  #CAFConfederationCup

𝗞𝗜𝗞𝗢𝗦𝗜 𝗖𝗛𝗔 𝗦𝗜𝗠𝗕𝗔 𝗗𝗛𝗜𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗚𝗘𝗡𝗗𝗔𝗥𝗠𝗘𝗥𝗜𝗘 𝗡𝗔𝗧𝗜𝗢𝗡𝗔𝗟𝗘

Image
 𝗞𝗜𝗞𝗢𝗦𝗜 𝗖𝗛𝗔 𝗦𝗜𝗠𝗕𝗔 𝗗𝗛𝗜𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗚𝗘𝗡𝗗𝗔𝗥𝗠𝗘𝗥𝗜𝗘 𝗡𝗔𝗧𝗜𝗢𝗡𝗔𝗟𝗘 1: Aishi Manula 2: Shomari Kapombe 3: Mohamed Hussein 4: Joash Onyango 5: Henock Inonga 6: Erasto Nyoni 7: Yusuph Muhilu 8: Sadio Kanoute 9: Medie Kagere 10: Pape Sakho 11: Peter Banda 𝗔𝗞𝗜𝗕𝗔 Beno, Ally, Israel, Kennedy,Bocco, Gadiel, Wawa,  Jimmyson, Morrison

Lukaku kavunja rekodi ya Epl !

Image
 Lukaku kavunja rekodi ya Epl !  - Kwa mara ya kwanza Epl mchezaji amecheza kwa dakika 90' na kufanikiwa kuugusa mpira mara saba tu !!! - Mchezaji huyo ni Lukaku !!! Aligusa mpira mara mbili tu kipindi cha kwanza jana dhidi ya Crystal palace. NB ; Akili iko Inter mwili uko Chelsea.

Ahmed Ally Watanzania Ondoeni Shaka Simba Sc Tunakuja Na Point Tatu

Image
Meneja Mawasiliano wa @simbasctanzania @ahmedally_ amesema wachezaji wote wako tayari kwa mchezo na ahadi waliyoitoa ni ushindi kwenye mechi ya leo dhidi ya USGN ya nchini Niger. "Wachezaji wote wapo timamu na wapo tayari kwa mchezo" "Kama kawaida yangu nimetembelea wachezaji wetu kuwajulia hali na kama haitoshi wametuhakikishia matokeo mazuri hii leo. Wana Simba wenzangu dua zenu ni muhimu sana kuelekea jioni ya leo" - Ahmed Ally

Masau Bwire Watanzania tuiombee ushindi Simba SC

Image
 ANAANDIKA MASAU BWIRE. *Watanzania tuiombee ushindi Simba SC*... Leo ni siku muhimu sana kwa ustawi wa Simba SC katika mashindano ya Shirikisho Afrika.  Matokeo chanya katika mchezo huo wa ugenini, yataongeza chachu na morari kwa wachezaji, viongozi, mashabiki,  wanachama wa Simba SC na Watanzania wazalendo katika kuifikisha timu hiyo hatua nyingine ya robo fainali ya mashindano hayo. Kufanikiwa kwa Simba SC na kufikia hatua ya juu ya mashindano hayo, ni heshima kubwa mno kwa Simba SC,  lakini ni heshima ya kipekee sana kwa nchi yetu kwa maendeleo ya soka letu. Kwa hali hiyo, niwaombe Watanzania wenzangu wote, tuache tofauti zetu, tuiombee Simba SC ifanye vyema katika mchezo wa leo Jumapili,  February 20, 2022, ipate ushindi ugenini, huko Niger dhidi ya USGN. Lakini pia niwaombe, kwa moyo wa kipekee kabisa,  tuiombee Ruvu Shooting,  katika mchezo wake wa leo, wa ligi kuu ya NBC,  dhidi ya Tanzania Prisons,  Sokoine, Mbeya, iweze kuibuka na u...

Friendly Match Yanga Sc Waitungua Cambiaso

Image
 🚨 FRIENDLY MATCH AVIC TOWN Yanga sc  5 v Cambiaso academy 1 Feitoo ⚽⚽ Mayele ⚽⚽ Chico ushindi ⚽.