KISINDA TUTAIPIGA SIMBA NYINGI
KISINDA TUTAIPIGA SIMBA NYINGI
Yule winga wa zamani wa Yanga SC 🇹🇿 kwenye kasi ya kishada, Tuisila Kisinda 🇨🇩 ambaye sasa anaitumikia klabu ya RS Berkane 🇲🇦, ameipiga mkwara Simba SC 🇹🇿 akidai hasira ya kipigo walichopewa na Asec Mimosas 🇨🇮 zitaishia kwao wakati timu hizo zitakapokutana katika mechi itakayopigwa Jumapili hii.
Kisinda amesema:
“Simba SC 🇹🇿 nawajua ni wazuri na matokeo waliyoyapata ugenini yamewapa nguvu, lakini nasi tumejipanga na tunataka ushindi dhidi yao bila kuangalia idadi ya mabao, tutawapiga.” alisema Kisinda ambaye kasi yake iliwasumbua sana mabeki wa Simba SC 🇹🇿 katika Kariakoo Derby.
Comments
Post a Comment